2 Corinthians 10:1-6

Paulo Atetea Huduma Yake

1 aBasi, mimi Paulo ninawasihi kwa unyenyekevu na upole wa Al-Masihi, mimi niliye “mwoga” ninapokuwa pamoja nanyi ana kwa ana, lakini mwenye ujasiri nikiwa mbali nanyi! 2 bNawaomba nitakapokuja kwenu nisiwe na ujasiri dhidi ya watu fulani, kama ninavyotazamia kwa wale wanaodhani kwamba tunaishi kwa kufuata namna ya ulimwengu huu. 3 cIngawa tunaishi duniani, hatupigani vita kama ulimwengu ufanyavyo. 4 dSilaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome, 5 etukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu, na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Al-Masihi, 6 ftena tukiwa tayari kuadhibu kila tendo la kutotii, kutii kwenu kutakapokamilika.

Copyright information for SwhKC